Sunday 10 March 2013

Rais Jakaya Kikwete
--
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jayaka KMrisho Kikwete amemtumia salamu za pongezi nyingi Rais Mteule wa Jamhuri ya Kenya, Mheshimiwa Uhuru Kenyatta.

Katika salamu hizo zilizotumwa leo, Jumamosi, Machi 9, 2013, saa chache baada ya kuthibitishwa rasmi kuwa Mheshimiwa Kenyatta ameshinda Uchaguzi Mkuu wa Kenya uliofanyika mwanzoni mwa wiki hii Jumatatu, Machi 4, 2013, Rais Kikwete amemwambia Mheshimiwa Uhuru Kenyatta:

“Mpendwa Rais Mteule na Kaka, ilikuwa ni furaha kubwa kwangu kupokea taarifa ya ushindi wako wa kuchaguliwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Kenya. Niruhusu, kwa niaba ya Serikali na Wananchi wa Tanzania, na kwa hakika, kwa niaba yangu binafsi kukupogenza kwa dhati ya moyo wangu kwa mafanikio haya makubwa ya kuchaguliwa kwako.”

Ameongeza Rais Kikwete: “ Ushindi huu ni ushahidi na ishara ya wazi kabisa ya imani na matumaini ambayo wananchi wa Kenya waliyonayo katika uongozi wako. Huu ni utambuzi wa kazi yako maridadi na mchango wako mkubwa ambao umeutoa katika nafasi mbali mbali za uongozi katika siku za nyuma katika jitihada zako za kuleta maendeleo ya kiuchumi na kijamii na ustawi wa nchi yako na wananchi wake.”

Amesisitiza Rais Kikwete: “Wakati unajiandaa kuchukua madaraka ya juu zaidi katika nchi yako, napenda kukuhakikishia msimamo wake binafsi pamoja na ule wa Serikali yangu wa kuunga mkono Serikali yako. Ni imani yangu kubwa kwamba pamoja tutaweza kuendelea kusukuma mbele zaidi maendeleo ya nchi zetu – Kenya na Tanzania na pia utengamano wa Afrika Mashariki kwa manufaa ya nchi zetu na wananchi wake.”



Imetolewa na:

Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais,

IKULU

DAR ES SALAAM

Results of Elections in Kenya


Press Statement
John Kerry
Secretary of State
Washington, DC
March 9, 2013



On behalf of the United States of America, I want to congratulate the people of Kenya for voting peacefully on March 4 and all those elected to office. Across the country, Kenyans turned out by the millions to exercise their most fundamental democratic right. I am inspired by the overwhelming desire of Kenyans to peacefully make their voices heard, and I applaud the patience they have shown as votes were tallied.
Foremost in our minds is a desire to see the will of the Kenyan people expressed freely and fairly. We strongly urge all parties and their supporters to peacefully address any disputes with today’s announcement by the Independent Electoral and Boundaries Commission through the Kenyan legal system, rather than on the streets. These elections are an historic opportunity for the people of Kenya to come together to build a better future. Since its independence in 1963, Kenya has been one of America’s strongest and most enduring partners in Africa. We stand with you at this historic moment and will continue to be a strong friend and ally of the Kenyan people.

No comments:

Post a Comment